www.kenethngamoga.blogspot.com

Bongofleva imepata msiba… John Woka amefariki alfajiri Dar es salaam

John Woka ni msanii ambaye Tanzania ilikuwa nae sana kwenye chati za muziki wa

bongofleva kupitia kundi la Watukutu, na sasa Tanzania imepata taarifa za kifo chake 

ilichotokea alfajiri ya February 16 ikiwa ni saa kadhaa tu

John Woka ni msanii ambaye Tanzania ilikuwa nae sana kwenye chati za muziki wa bongofleva kupitia kundi la Watukutu, na sasa Tanzania imepata taarifa za kifo chake kilichotokea alfajiri ya February 16 ikiwa ni saa kadhaa tu baada ya kupelekwa Hospitali.
Woka amefariki baada ya kupata ajali  wakati anatengeneza gari Sinza kwenye mfumo wa AC inasemekana kuna kitu kilifyetuka baada ya kufungua AC na kumpiga kwenye paji la uso na kuingia kama inchi 3 au 2 hivyo damu nyingi zikaanza kumtoka kichwani na mpaka anafikishwa hospitali, Woka alikuwa katika chumba cha wagonjwa Mahututi.
Kifo cha John Woka ni pengo jingine kwenye bongofleva, alipita kwenye chati mbalimbali za muziki huu kutokana na nyimbo zake kama mganga na hii kitu hii ambazo alizipiga kwa kurap kama mlevi
SIKILIZA MOJA YA NYIMBO ZA JOHN WOKA HAPA CHINI

Ungana na mimi kupitia Facebook , Twitter na Instagram Pia subscribe Youtube ili uwe wa kwanza kupata habari mpya.
Share on Google Plus

Keneth Ngamoga

Keneth Ngamoga ni mtangazaji wa radio Pambazuko iliyopo Ifakara.Huwa akisikika katika vipindi tofauti vya burudani.Kwa msaada na ushauri Wasiliana na Keneth Ngamoga Kupitia namba
+255655632798
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment