PICHA ya staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ ikimuonesha akiwa amelala ameshikilia tuzo, imezua gumzo mitandaoni huku kila mmoja akimpongeza na wengine kufananisha staili hiyo kuwa imeshawahi kutumiwa na nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta na
Elizabeth Michael ‘Lulu’
PICHA ya staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ ikimuonesha akiwa amelala ameshikilia tuzo, imezua gumzo mitandaoni huku kila mmoja akimpongeza na wengine kufananisha staili hiyo kuwa imeshawahi kutumiwa na nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta na staa wa Bongo Fleva, Diamond.
Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ambaye naye aliwahi kupozi pozi hilo akiwa na tuzo za MTV.
Lulu ambaye usiku wa kuamkia Jumapili katika sherehe za utoaji tuzo za African Magic Viewers Choice 2016 aliibuka kidedea kwa kushinda Tuzo ya Filamu Bora Afrika Mashariki (Mapenzi).
Miongoni mwa meseji zilizozua gumzo baada ya kuposti picha hiyo ni;
“Namtafuta aliyekupiga picha?”
Mbwana Samatta akiwa kalala na tuzo yake ya Mchezaji Bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza Afrika.
“Pozi la Taifa.”
“That’ z our style after achieve it.”
“Tayari hukuuu pic kama ya zilee tuzo zetu nyingine.”
Usiku huo pia, staa mwingine wa filamu, Richie Mtambalike alifanikiwa kushinda katika kipengele cha Filamu Bora ya Kiswahili (Kitendawili).
SHARE NA WASHIKAJI
Ungana na mimi kupitia
Facebook ,
Twitter na
Instagram Pia subscribe
Youtube ili uwe wa kwanza kupata
habari mpya.
Keneth Ngamoga ni mtangazaji wa radio Pambazuko iliyopo Ifakara.Huwa akisikika katika vipindi tofauti vya burudani.Kwa msaada na ushauri Wasiliana na Keneth Ngamoga Kupitia namba
+255655632798
0 comments:
Post a Comment