www.kenethngamoga.blogspot.com

KAULI YA KWANZA YA MKWASA BAADA YA KUKANYAGA ARDHI YA TANZANIA AKITOKEA CHAD (Audio)


Timu ya taifa ya Tanzania imewasili March 25 (leo Ijumaa) alfajiri ikitokea nchini Chad, baada ya timu hiyo kuwasili shaffihdauda.co.tz ilijitahidi kutafuta nafasi ya kuzungumza na nahodha wa kikosi hicho Mbwana Samatta lakini muda mwingi alikuwa ametingwa na mashabiki waliomlaki kwa shangwe kufuatia kuisaidia Stars kupata ushindi wa ugenini.
Baada ya mambo kuwa magumu kuzungumza na Samatta ili kutaka kujua mambo kadhaa kuhusiana na mchezo uliopita na ule wa marudiano, moja kwa moja ikabidi shaffihdauda ifanye mahojiano na kocha mkuu wa timu kutaka kujua malengo na mikakati yake kuelekea mchezo wa marudiano.

“Game ya nyumbani najua itakuwa ngumu kwasababu Chad ni wazuri wanawachezaji professionals wanacheza kwa kujiamini na wakija kucheza hapa watacheza kwa kujiachia kwahiyo mechi itakuwa ngumu”, anasema Mkwasa ambaye uso wake unaonesha kufurahishwa na matokeo ya ushindi wa ugenini licha ya kusisitiza mchezo ulikuwa mgumu kutokana na hali ya hewa na ubora wa wapinzani wake.
“Wao wanaimani wanaweza wakapata ushindi kama walivyowahikupata ushindi katika kipindi kilichopita, lakini na sisi tumejipanga kuhakikisha historia haijirudii, kama walitufunga mara ya kwanza kwetu sisi tumeamua kupata ushindi mwingine tukiwa nyumbani.
“Nawaomba watanzania waje kwa wingi ku-support wachezaji na wawe pamoja na wachezaji watuombee kwa Mungu”.
“Timu imerejea ikiwa na majeruhi wawili ambao ni Mwinyi Kazimoto na Kelvin Yondani ambaye alipata matatizo baada ya mechi lakini wote wanaendelea vizuri, ndiyo kwanza tumerudi daktari wa timu ataangalia na atatupa taarifa kamili itakuwaje”.
Stars itacheza mchezo wa marudiano dhidi ya Chad March 28 siku ya Jumatatu ya Pasaka kwenye uwanja wa taifa, Dar es Salaam.
Dondoka hapa chini umsikilize mwenyewe Mkwasa anavyofunguka kuhusu mchezo wamarudiano dhidi ya Chad utakaopigwa taifa

Ungana na mimi kupitia Facebook , Twitter na Instagram Pia subscribe Youtube ili uwe wa kwanza kupata habari mpya.
Share on Google Plus

Keneth Ngamoga

Keneth Ngamoga ni mtangazaji wa radio Pambazuko iliyopo Ifakara.Huwa akisikika katika vipindi tofauti vya burudani.Kwa msaada na ushauri Wasiliana na Keneth Ngamoga Kupitia namba
+255655632798
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment