www.kenethngamoga.blogspot.com

Beyonce ‘Lemonade’ yashtakiwa kwa kuiba kazi ya kisanaa

Albamu mpya ya Lemonade iliotolewa na Beyonce Knowles imeorodheshwa miongoni mwa albamu zilizopendwa sana baada ya kutolewa mwaka huu,lakini ,kipande cha albamu hiyo kilichotolewa wiki moja kabla ya uwepo wa albamu hiyo kufichwa hadi wakati wa toleo la filamu fupi lililoandamana na albamu hiyo kimezua utata.
Kipande hicho cha albamu hiyo kilishirikisha msururu wa vipande vifupi vifupi vya albamu hiyo bila maelezo ,vingi vikimuonyesha Beyonce na kumalizika kwa maelezo yaliosema :Lemonade A world Permier event.
Na sasa mtengezaji huru wa filamu kwa jina Matthew Fulks anadai kuwa kipande hicho kilinakili mojawapo ya kazi zake kwa jina Palinoia.
Fulks anadai kwamba kampuni ya muziki ya Sony ile ya Columbia Recordings pamoja na ile ya Beyonce Parkwood Entertainment zilijua kuhusu kazi yake kabla ya utengezaji wa Lemonade ulipoanza na kwamba walishawishiwa na kazi yake.
Anasema kuwa kipande hicho cha albamu ya Lemonade kinafanana na kile cha Palinoia ambayo ni kazi yake.
Anaongezea kuwa baadhi ya vitu vinavyofanana kati ya filamu hizo mbili ni pamoja na michoro katika ukuta,watu wenye macho mekundu na picha zilizopigwa katika ngazi pamoja na eneo la kuegesha magri chini ya nyumba.
Ungana na mimi kupitia Facebook , Twitter na Instagram Pia subscribe Youtube ili uwe wa kwanza kupata habari mpya.
Share on Google Plus

Keneth Ngamoga

Keneth Ngamoga ni mtangazaji wa radio Pambazuko iliyopo Ifakara.Huwa akisikika katika vipindi tofauti vya burudani.Kwa msaada na ushauri Wasiliana na Keneth Ngamoga Kupitia namba
+255655632798
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment