
1- Ureno wanaingia kucheza mchezo wa fainali ya Euro 2016, wakiwa na rekodi ya kufungwa mechi zao 10 za mwisho mfululizo dhidi ya Ufaransa.
2- Ureno na Ufaransa wamecheza jumla ya mechi 24, Ureno amewahi kumfungaUfaransa mara 5 na kutoka sare mara 1, huku akiwa ameruhusu kufungwa mara 18.

3- Mara ya mwisho Ureno kumfunga Ufaransa ilikuwa ni April 26 1975 kwa goli 2-0 katika mchezo wao wa kimataifa wa kirafiki, yaani imepita miaka 41.
4- Hii itakuwa fainali ya 17 kwa Cristiano Ronaldo kucheza katika maisha yake ya soka, ameshinda jumla ya fainali 11 kati ya 16 ambazo tayari ameshacheza.
5- Antoine Griezmann ndio mchezaji anayeshikilia rekodi ya ufungaji bora wa muda wote katika hatua ya mtoano, akiwa kafunga jumla ya goli 5.

0 comments:
Post a Comment