www.kenethngamoga.blogspot.com

Kutana na mwanamke mnene kuliko wote duniani… Ana uzito wa kilo 500

Kazi yangu ni kuhakikisha kila siku nakuletea habari mpya na uhakika popote ulipo mtu wangu na nimekula kiapo kwako kulitekeleza hilo na leo nimeipata hii kutoka nchini Misri kuhusu Mwanamke mnene kuliko wote duniani ambaye anatajwa kufikisha uzito wa kilo 500.

Kazi yangu ni kuhakikisha kila siku nakuletea habari mpya na uhakika popote ulipo mtu wangu na nimekula kiapo kwako kulitekeleza hilo na leo nimeipata hii kutoka nchini Misri kuhusu Mwanamke mnene kuliko wote duniani ambaye anatajwa kufikisha uzito wa kilo 500.
Kwa mujibu wa jarida la Daily Mail, inaelezwa kuwa mwanamke huyo aitwaye Iman Ahmad Abdulati mwenye miaka 36 hajawahi kutoka ndani kwa miaka 25 na amekua akiongezeka uzito wake kwa haraka mpaka kufikia kilo 500 zinazompa shida ya kujifanyia usafi na hata kula. Ripoti ya madaktari inaonesha kuwa mwanamke huyu anasumbuliwa na maambukizi ya bakteria wanaoshambulia ukuaji wa mwili.
Akiwa na miaka 11 alianza kusumbuliwa na tatizo hilo ingawa wazazi wake wanakiri kuwa hawakudhani kuwa ni tatizo lakini siku zilivyozidi kwenda ndipo wakabaini kuwa halikua jambo la kawaida hivyo wakaamua kutafuta wataalamu ambao walitoa ripoti kuwa ana matatizo ya mwili wake kukaa na maji mengi bila kuyatoa nje kitu ambacho sio cha kawaida kwa binadamu.
Ungana na mimi kupitia Facebook , Twitter na Instagram Pia subscribe Youtube ili uwe wa kwanza kupata habari mpya.
Share on Google Plus

Keneth Ngamoga

Keneth Ngamoga ni mtangazaji wa radio Pambazuko iliyopo Ifakara.Huwa akisikika katika vipindi tofauti vya burudani.Kwa msaada na ushauri Wasiliana na Keneth Ngamoga Kupitia namba
+255655632798
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment