www.kenethngamoga.blogspot.com

Video 'yaonyesha wasichana wa Chibok waliotoweka'

Kundi la kigaidi la Boko Haram limetoa kanda ya video, wanayodai inaonyesha wasichana waliotekwa nyara katika eneo la Chibok miaka miwili iliyopita.

Wasichana wa Chibok waliotekwa nyara
Image captionWasichana wa Chibok waliotekwa nyara
Video hiyo, inamuonyesha mwanamume mmoja aliyejifunika uso wake, akiwa amejihami kwa silaha, akizungumza na kundi la wanawake takriban 50.
Wote wamevalia mavazi ya kidini.
Mmoja wa wanawake hao anajitambulisha kuwa, Madia na kusema kuwa anatoka Chibok.
Anasema wenzake kadhaa wamejeruhiwa vibaya kutokana na mashambulizi ya angani ya wanajeshi wa Nigeria.
Anatoa wito kwa serikali kuwaachilia wanachama wa Boko Haram, ili wasichana hao waachiliwe huru.
Inaonekana kuwa Boko Haram inatumia video hiyo kuwafanya raia wa Nigeria kuwahurumia wasichana hao, na kuilazimu serikali kutimiza matakwa yao.
Serikali ya Nigeria haijasema lolote kuhusiana na video hiyo.
BBC
Ungana na mimi kupitia Facebook , Twitter na Instagram Pia subscribe Youtube ili uwe wa kwanza kupata habari mpya.
Share on Google Plus

Keneth Ngamoga

Keneth Ngamoga ni mtangazaji wa radio Pambazuko iliyopo Ifakara.Huwa akisikika katika vipindi tofauti vya burudani.Kwa msaada na ushauri Wasiliana na Keneth Ngamoga Kupitia namba
+255655632798
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment