www.kenethngamoga.blogspot.com

VIDEO:Ufaransa vs Iceland 5_2

Hatimae usiku wa July 3 2016 michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya 2016 hatua ya robo fainali ilimalizika rasmi kwa robo fainali ya mwisho kupigwa katika uwanja wa Stade de France ukizikutanisha mwenyeji wa michuano hiyo kwa mwaka 2016 timu ya taifa yaUfaransa dhidi ya timu ya taifa ya Iceland.
Hatimae usiku wa July 3 2016 michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya 2016 hatua ya robo fainali ilimalizika rasmi kwa robo fainali ya mwisho kupigwa katika uwanja wa Stade de France ukizikutanisha mwenyeji wa michuano hiyo kwa mwaka 2016 timu ya taifa yaUfaransa dhidi ya timu ya taifa ya Iceland.
Katika mchezo huo uliotazamiwa kupata mashabiki zaidi ya 60000, ulimalizika kwa timu ya taifa ya Ufaransa kuondoka na ushindi mnono wa magoli 5-2, magoli ya Ufaransayalifungwa na Oliver Giroud dakika ya 13 na 59, Paul Pogba dakika ya 20, Dimitri Payet dakika ya 43 na Antoine Griezmann dakika ya 45.
Wakati timu ya taifa ya Iceland ilifanikiwa kuondoka na magoli mawili pekee yaliofungwa na Kolbeinn Sigporsson dakika ya 56 na Birkir Bjarnason dakika ya 84. Kwa matokeo hayo sasa ni rasmi timu ya taifa ya Ufaransa itacheza dhidi ya timu ya taifa ya Ujerumanikatika mchezo wa nusu fainali ya Euro 2016
Ungana na mimi kupitia Facebook , Twitter na Instagram Pia subscribe Youtube ili uwe wa kwanza kupata habari mpya.
Share on Google Plus

Keneth Ngamoga

Keneth Ngamoga ni mtangazaji wa radio Pambazuko iliyopo Ifakara.Huwa akisikika katika vipindi tofauti vya burudani.Kwa msaada na ushauri Wasiliana na Keneth Ngamoga Kupitia namba
+255655632798
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment