Kwa jina anaitwa Nkosinathi Innocent Maphululo, alizaliwa eThekwini huko Afrika ya Kusini, tarehe 11 machi 1976, ana mke ambaye na yeye ni Muigizaji na mtangazaji wa Televisheni, na ana watoto wanne (4), wawili kutoka katika mahusiano yake ya zamani na wawili kutoka kwa mkewe wa ndoa. Black Coffee ni DJ, Mtayarishaji wa muziki, mwimbaji na vile vile ni mfanyabiashara,
Alisomea masomo ya Jazz katika chuo cha Technikon Natal kabla hajawa mwitikiaji wa nyimbo za Madala Kunene akiwa na wenzie waliosoma wote. Baadae walianzisha kikundi chao wenyewe cha Afro-pop kilichoitwa Shana. Black Coffe alichaguliwa kuwa mmoja kati ta washiriki wawili kutoka South Afrika kwenye Red Bull Music Academy mwaka 2003 iliyomsadia kuingia katika South African dance music scene. Muziki wake wa kwanza uliitwa ‘Hapiness’ na ulishirikishwa kwenye albamu ya kazi za MaDj.
Licha ya nyimbo moja moja alizotoa, pia Black Coffee ana albamu zifatazo:
  • Black Coffee(Soulistic Music, 2005)
  • Have Another One(Soulistic Music, 2007)
  • Home Brewed(Soulistic Music, 2009)
  • Africa Rising DVD(Soulistic Music, 2012)
  • Africa Rising CD(Soulistic Music, 2012)
  • Pieces of Me(Soulistic Music 2015)
Tuzo nyingine alizowahi kupokea ni
2005 – SAMA Best Urban Dance Album
2010 – South African Music Awards#12th South African Music Awards .282006.29
2010 – SAMA Best Male Artist
2010 – Health Magazine Best Man
2010 – Metro FM Award for Best Produced Album
2010 – Metro FM Award for Best Dance Album
2011 – Channel O Award for Most Talented Male Artist
2012 – Sunday Times Generation NEXT Award for Coolest DJ
2013 – SAMA Best Dance Album
2013 – Sunday Times Generation NEXT Award For Coolest DJ 2013
2014 – Sunday Times Generation Next Award for Coolest DJ
2015 – DJ Awards for Breakthrough DJ Of The Year
2016 – SAMA Best Dance Album