
Rais Mh. Dk. John Pombe Magufuli akila kiapo mbele ya Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Mohamed Chande kwenye uwanja wa Uhuru leo kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mara baada ya kushinda uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni, Rais Dk. John Pombe Magufuli ameapa katika sherehe iliyohudhuriwa na marais mbalimbali wa Afrika wakiwemo Robert Mugabe wa Zamibabwe, Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Joseph Kabila wa DRC Congo, Paul Kagame wa Rwanda, Yoweri Museveni wa Uganda, Uhuru Kenyata wa Kenya, Philipe Nyusi wa Msumbiji, Edgar Lungu wa Zambia na wengine wengi wakiwemo mabalozi wa mataifa ya Ulaya, Marekani na taasisi za kimataifa ambao wameshuhudia sherehe hizo.
Dk.John Pombe Magufuli anakuwa rais wa awamu ya tano baada ya kupokea kijiti kwa watangulizi wake Hayati Baba wa Taifa Mwalimu J.K.Nyerere, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mzee Benjamin Mkapa na sasa Dk. Jakaya Kikwete ambaye ndiye aliyemuachia kijiti Dk. Magufuli.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
Rais Dk. John Pombe Magufuli akipokea vitendea kazi kutoka kwa Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Mohamed Chande mara baada ya kuapishwa kwenye uwanja wa Uhuru leo, anayeshuhudia kushoto ni Rais Mstaafu Dk. Jakaya Kikwete.
Rais Dk. John Pombe Magufuli akipokea silaha za kijadi kutoka kwa mmoja wa wazee Mzee Job Lusinde mara baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ungana na mimi kupitia
Facebook ,
Twitter na
Instagram Pia subscribe
Youtube ili uwe wa kwanza kupata
habari mpya.
Keneth Ngamoga ni mtangazaji wa radio Pambazuko iliyopo Ifakara.Huwa akisikika katika vipindi tofauti vya burudani.Kwa msaada na ushauri Wasiliana na Keneth Ngamoga Kupitia namba
+255655632798
0 comments:
Post a Comment